Thursday, June 24, 2010

DAWA YA WABAKAJI YAGUNDULIKA

RAPE-AXE


Dr. Sonnet Ehlers amesema anahakikisha anasambaza condom mpya alizozitengeneza 30,000 zenye meno muda huu wa world cup maalum kwajili ya wabakaji maana wamekithiri nchini humo.Condom hizo zinajulikana kama RAPE-AXE na mara baada ya kipindi hiki cha mgao wa bure zitakuwa zinauzwa kwa dolla 2.
condom hizo anazivaa mwanamke pale ambapo atakuwa hanauhakika na usalama wa sehemu anayoenda na mbakaji akitokea kumbaka inamkaba kama mtego wa panya . Dr huyo anasema inauma sana, atashindwa kukojoa wala kutembea, akijaribu kuitoa ndivyo itavyozidi kumbana ila haichubui ngozi, na ni mpaka afanyiwe operation ndio iweze kutolewa. DR SONNET ANAAMINI ITASAIDIA SANA MAMLAKA KUWACHUKULIA HATUA WABAKAJI.

Blog Archive